Biden aapa kumshinda Trump baada ya kuyumba mwenye mdahalo

Rais Biden anasema hangeligombea muhula wa pili iwapo hangeweza kufanya kazi hiyo, baada ya utendakazi wake kuzua wasiwasi miongoni mwa wanachama wa Democratic.

Muhtasari

  • Afisa wa Serbia afumwa mshale nje ya ubalozi wa Israel
  • M23 wauteka mji wa Kanyabayonga mashariki kwa DR- Congo
  • Meneja wa kiwanda cha chai aliyeangaziwa katika BBC Africa Eye achaguliwa Mkurugenzi
  • Wanajeshi kudumisha usalama Kenya hadi utulivu utakaporejea
  • Biden aapa kumshinda Trump baada ya kuyumba mwenye mdahalo

Moja kwa moja

Ambia Hirsi

  1. Afisa wa Serbia afumwa mshale nje ya ubalozi wa Israel

    Polisi huyo alimpiga risasi mshambuliaji huyo na kumuua baada ya kujeruhiwa shingoni

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Polisi huyo alimpiga risasi mshambuliaji huyo na kumuua baada ya kujeruhiwa shingoni

    Afisa wa polisi wa Serbia amejeruhiwa katika shambulio la mshale nje ya ubalozi wa Israel mjini Belgrade.

    Waziri wa Mambo ya Ndani Ivica Dacic aliwaambia waandishi wa habari kwamba afisa huyo alimpiga risasi na kumuua mshambuliaji.

    Mshambuliaji huyo - ambaye bado hajatambuliwa na mamlaka - alimfuma polisi mshale shingoni, Bw Dacic alisema.

    Afisa huyo amepelekwa hospitalini kufanyiwa upasuaji kutibu jeraha lake, na inasemekana yuko katika hali mbaya.

    Shirika la utangazaji la Serbia B92 alimnukuu Bw Dacic akisema kwamba mshambuliaji alikaribia jengo dogo mbele ya ubalozi wa Israel mwendo wa 11:00 (09:00 GMT), akidaiwa kuuliza kuhusu jumba la makumbusho.

    Mwanamume huyo alikuwa amefungua mlango wa jengo hilo dogo, akatoa upinde na na mshale na kumfuma afisa huyo, Bw Dacic aliripotiwa kusema.

    Bw Dacic alisema tukio hilo linachunguzwa na waendesha mashtaka maalum na kwamba wengine kadhaa wamekamatwa kama hatua ya tahadhari.

    Sio mara ya kwanza kwa mtu kujaribu kufanya shambulio kwenye ubalozi wa Israeli huko Belgrade tangu vita vya Gaza ambavyo Israeli ilianza baada ya shambulio la Hamas la 7 Oktoba kusini mwa Israel.

  2. M23 wauteka mji wa Kanyabayonga mashariki kwa DR- Congo

    Wapiganaji wa M23 wamesababisha uharibifu mkubwa masharki mwa DR Congo

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wapiganaji wa M23 wamesababisha uharibifu mkubwa masharki mwa DR Congo

    Waasi wa M23 wameuteka mji wa kimkakati wa Kanyabayonga mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mapema Jumamosi baada ya mapigano makali na vikosi vya Congo

    Waasi hao walichukua udhibiti wa maeneo mawili kabla ya kuuteka Kanyabayonga, mji muhimu ulioko kati ya vituo vikuu vya kibiashara vya Butembo na Beni kaskazini mwa nchi hiyo.

    Afisa mmoja wa eneo hilo aliripoti kuwa wakazi walikimbia makazi yao mwendo wa alfajiri wakati waasi wakianzisha mashambulizi yao.

    Kanyabayonga imekuwa kimbilio la maelfu ya watu ambao wamekimbia kutoka kwa waasi katika miezi ya hivi karibuni.

    Mkoa wa Kivu Kaskazini umekumbwa na ghasia tangu 2021, wakati M23 walipoanzisha tena mashambulizi yao.

    Kinshasa imefutilia mbali mazungumzo yoyote na M23.

    Kwa pamoja na Umoja wa Mataifa, inaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi, madai ambayo Kigali inakanusha.

    Maelezo zaidi:

  3. Meneja wa kiwanda cha chai aliyeangaziwa katika BBC Africa Eye achaguliwa Mkurugenzi

    Msimamizi wa shamba la majani chai aliyeangaziwa katika ufichuzi wa BBC Africa Eye na Panorama nchini Kenya kuhusu sakata ya unyanyasaji wa kingono, amechaguliwa kuwa mkurugenzi wa Mamlaka ya chai nchini licha ya pingamizi ya umma dhidi ya ugombea wake.

    John Chebochok alishinda nafasi ya mkurugenzi mteule wa Mamlaka ya Maendeleo ya Chai Kenya (KTDA). Sasa atasimamia ukanda wa Ainamoi huko Kericho, kusini-magharibi mwa Kenya.

    Kaunti ya Kericho inajulikana kuwa na mashamba makubwa zaidi ya chai nchini Kenya.

    Pia hukuza baadhi ya chapa maarufu za chai nchini Kenya na Uingereza.

    Bw. Chebochok alishinda kwa kura 526 dhidi ya kura 356 za mpinzani wake.

    Uchaguzi huo, ambao uliandaliwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), awali ulipangwa kufanyika katika viwanda 54 vya wakulima wadogo wa chai kote nchini mnamo Ijumaa, 28 Juni. Lakini, iliishia kufanyika katika viwanda vichache.

    KTDA ilisema ucheleweshaji huo ulitokana na hitilafu ya utayarishaji na utoaji wa vifaa vya uchaguzi.

    Upigaji kura utaendelea katika viwanda vingine vya chai, leo Jumamosi.

    Baadhi ya Wakenya mtandaoni wameeleza kuwa uchaguzi wa Bw Chebochok ni tishio kwa uadilifu wa sekta ya chai.

    "Tunaelezea shutuma zetu zisizo na shaka juu ya uwezekano wa kuchaguliwa kwa Bw. John Chebochok kama Mkurugenzi wa Kiwanda cha Chai cha Toror kinachosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Chai la Kenya, licha ya tuhuma ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake uliofichuliwa na kitengo cha uchunguzi cha BBC mnamo Februari 2023," taarifa ya Chama cha Wanawake katika sekta ya Majani Chai Kericho, ilisema kbala ya uchaguzi.

  4. Wanajeshi kudumisha usalama Kenya hadi utulivu utakaporejea

    Wanajeshi

    Waziri wa Ulinzi wa Kenya ameapa kuwa wanajeshi wataendela kushika doria mitaani hadi hali ya kawaida itakaporejea baada ya wiki moja ya machafuko ya kisiasa.

    Nchi hiyo ya Afrika Mashariki inajiandaa kwa duru mpya ya maandamano wiki ijayo, kuendeleza maandamano yaliyomlazimu Rais William Ruto kusitisha mapendekezo ya nyongeza ya ushuru.

    Muda mfupi baada ya jaji kuamuru vikosi vya usalama kutotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji, Waziri wa Ulinzi wa Kenya alitangaza kwamba jeshi litatumwa kusaidia polisi ambao walikuwa wamezidiwa na waandamanaji.

    Waziri Duale alisema hatua hiyo ni ya kujibu dharura ya usalama iliyosababishwa na maandamano ya kitaifa ambayo yaligeuka kuwa ya vurugu.

    Kulingana na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, takribani watu 30 waliuawa wakati polisi walipowafyatulia risasi waandamanaji mapema wiki hii.

    Shirika hilo linadai kuwa vikosi vya usalama vililenga waandamanaji waliokuwa wakijaribu kukimbia.

    Vijana hao waandamanaji wanataka kuondolewa kwa kazi zilizotolewa kinyume na katiba, kuondolewa kwa kodi zingine, na kufutwa kazi kwa maafisa wa umma walio na rekodi za uhalifu.

    Pia soma:

  5. Biden aapa kumshinda Trump baada ya kuyumba mwenye mdahalo

    Biden

    Chanzo cha picha, EPA

    Rais wa Marekani Joe Biden amejibu shutuma zinazotolewa kuhusu umri wake, na kuwahakikishia wafuasi wake kwamba atashinda tena uchaguzi wa Novemba baada ya kutofanya vyema katika mdahalo wa urais uliozua wasiwasi kuhusu hali yake.

    "Najua mimi si kijana, kusema kweli," alisema katika mkutano huko North Carolina siku ya Ijumaa, siku moja baada ya kuhangaika katika mpambano wa televisheni na mpinzani wake wa Republican Donald Trump.

    "Sitembei kirahisi kama nilivyokuwa zamani... Sijadili kama nilivyokuwa nikijadili," alikiri. "Lakini ninachojua, kwa hakika ...najua jinsi ya kufanya kazi hii."

    Bw Biden, 81, alisema anaamini kwa "moyo mmoja" kwamba angeweza kuhudumu muhula mwingine, huku umati wa watu waliokuwa wakishangilia mjini Raleigh wakisema kwa sauti "four more years”, kumaanisha miaka minne zaidi.

    Wakati huo huo, Trump alifanya mkutano wa aina yake huko Virginia saa chache baadaye, ambapo alisifia "ushindi wake mkubwa" katika mjadala huo, ambao CNN ilisema ulitazamwa na watu milioni 48 kwenye televisheni na mamilioni zaidi mtandaoni.

    "Tatizo la Joe Biden sio umri wake," Trump mwenye umri wa miaka 78 alisema. "Ni uwezo wake. Hana uwezo kabisa.

    Rais huyo wa zamani alisema haamini uvumi kwamba Bw Biden angejiondoa katika kinyang'anyiro hicho, akisema "anafanya vyema zaidi katika uchaguzi" kuliko wagombea wengine wa Democratic, akiwemo Gavana wa California Gavin Newsom na Makamu wa Rais Kamala Harris.

    Maelezo zaidi:

  6. Natumai hujambo.