Ulaya ya Kaskazini
Mandhari
![](https://cdn.statically.io/img/upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/6b/Northern-Europe-map-extended.png/280px-Northern-Europe-map-extended.png)
![](https://cdn.statically.io/img/upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/08/United_Nations_geographical_subregions.png/520px-United_Nations_geographical_subregions.png)
Ulaya ya Kaskazini ni sehemu ya kaskazini ya bara la Ulaya. Kuna maelezo ya kutofautiana ni nchi zipi ambazo ni sehemu ya kanda hili.
Kwa hakika tamko hili lamaanisha:
- Nchi za Skandinavia pamoja na Denmark, Ufini, Iceland, Norwei na Uswidi, pia visiwa vya Faroe.
- Nchi za Kibalti yaani Estonia, Latvia na Lithuania.
- Mara nyingi ama sehemu ya kaskazini ya Britania (=Uskoti) au funguvisiwa ya Britania yote huhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya ya kaskazini yaani Uingereza, Uskoti, Welisi, Ueire na kisiwa cha Man.
- Wakati mwingine hata nchi nyingine kando la Bahari ya Baltiki kama Urusi ya kaskazini-magharibi, Poland ya kaskazini, Ujerumani ya Kaskazini zinahesabiwa humo.