Watazamaji nyota kote ulimwenguni walipata fursa ya kujionea Mwezi mpevu na mkubwa kuliko kawaida Jumanne usiku.
Mwezi huu mpevu, unaoitwa Mwezi wa Sturgeon, uliangaza anga la usiku ulipopaa juu ya upeo wa macho muda mfupi baada ya jua kutua.
Ni mwezi wa kwanza kati ya miandamo miwili ya mwezi huu - mwezi mpevu ujao utaonekana tarehe 30 Agosti utaitwa Mwezi wa Bluu ukiwa ni mwezi mpevu wa pili kuonekana katika mwezi mmoja wa kalenda.
Hizi ni baadhi ya picha bora za mwezi mpevu wa Jumanne kutoka kote duniani: